jeremiah_mpina

jeremiah_mpina Tourism

14/05/2023

Chui ni paka wakubwa wazuri na wenye nguvu wanaohusiana kwa karibu na Simba, Simbamilia, na Jaguar. Wanaishi Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, kaskazini-mashariki mwa Afrika, Asia ya Kati, India, na China. Hata hivyo, wengi wa makazi yao wako hatarini, hasa nje ya Afrika.

Ujuzi wa Uwindaji
Chui ana nguvu nyingi na anastarehe kwenye miti hivi kwamba mara nyingi husafirisha/kupansisha mauaji yake/windo lake juu ya Miti. Kwa kuburuza miili ya wanyama wakubwa juu juu huwaweka kuwaweka salama kutokana na wawindaji wengine k**a vile Fisi, ambao huwa na tabia ya kunyang'anya Chakula kutoka kwa Windaji wengine k**a Chui, Simba n.k.

Chui pia wanaweza kuwinda kutoka juu miti, ambapo makoti yao yenye madoadoa (Camouflage) huwaruhusu kuchanganyikana na majani hadi watokeze kwa kishindo cha kuua (Deadly pounce).

Chui pia huwinda nyakati za usiku, huwanyemelea swala, na nguruwe pori (Ngiri) kwa kuzunguka-zunguka kwenye nyasi ndefu. Na wakati mwingine kwenye makazi ya watu yalipo, Chui mara nyingi hushambulia mbwa na mara kwa mara watu pia.

Chui ni waogeleaji hodari na huwa nyumbani sana majini, ambapo wakati mwingine hula samaki au kaa. Kutokana na uhodari Uwindaji wake Chui inamfanya kuwa Predator mwenys kisasi dhidi ya Predators wenzake .

NATURE IS BEAUTIFUL 💖💖💖, NATURE IS INCREDIBLE 💖💫💫💫

🇹🇿

11/05/2023

URUTUBISHO KWA WANYAMA. Kurutubisha kwa wanyama ni mchakato wa kibayolojia unaohusisha mbegu ya kiume (gamete ya kiume/male gamete) kuunganishwa na yai (gamete jike au ovum/female gamete). Kuna aina tatu (03) ya urutubisho wa Wanyama.

🌍 OVIPAROUS/OVIPARITY.
Ni aina ya urutubisho ya Wanyama wanaotaga mayai. Wanyama wa oviparous hutoa mayai ambayo baadaye huanguliwa kwa mtoto baada ya kutolewa nje ya mwili wa jike. Mfano mamalia, Ndege, Mijusi n.k wana mayai ya uzazi.

🌍 VIVIPAROUS/VIVIPARITY.
Ni wanyama ambao kurutubishwaji na ukuaji wa kiinitete hutokea ndani ya tumbo la mama. Viviparity ni aina ya uzazi inayopatikana katika mamalia wengi na katika spishi zingine kadhaa. Wanyama wa Viviparous huzaa watoto wanaoishi ambao wamelishwa karibu na miili ya mama zao, hapa tunazungumzia Placenta. Mfano Binadamu, Nyani, Mbwa, na Paka ni wanyama viviparous.

🌍 OVOVIVIPAROUS/OVOVIVIPARITY.
Katika wanyama wa ovoviviparous, urutubisho wa yai hufanyika ndani, kwa kawaida k**a matokeo ya kuunganishwa. Wanyama wa Ovoviviparous huendeleza au kukuza watoto wao ndani ya yai katika mwili wao, lakini mtoto huzaliwa akiwa hai. Kiinitete hulishwa na kiini cha yai k**a ilivyo kwa wanyama walio na oviparous. Yai litaanguliwa ndani ya mwili wa mzazi na kisha mtoto kuzaliwa akiwa hai.

SPOTTED HYENAFisi jike ni mkubwa kimwili na mwenye Nguvu zaidi kuliko Fisi Dume, maumbile ya Fisi jike pia hufanana sana...
08/05/2023

SPOTTED HYENA

Fisi jike ni mkubwa kimwili na mwenye Nguvu zaidi kuliko Fisi Dume, maumbile ya Fisi jike pia hufanana sana na ya Fisi Dume, na Watu wengi hudhani kwamba Fisi jike ana jinsia mbili lakini siyo kweli ukweli upo hivi maumbile ya Fisi jike yanatofautiana sana na maumbile ya Wanyama wengine k**a Simba, Mbwa wa kufugwa, Mbwa Mwitu, Mbuzi, Kondoo, Ng'ombe na Wanyama wengine ambao wote Virginia zao zipo nyuma lakini Fisi jike ana tubelike-pseudo p***s (long-elongated cl****is) ambayo ni fake p***s ambayo hai-erect k**a Fisi Dume, ambayo husababisha suala la kujamiiana na dume na kuzaa kuwa na maumivu makali zaidi.

Fisi jike pia yeye ndio Kiongozi kwenye kundi lake na kundi la Fisi huitwa Ukoo (Clan). Na Fisi Dume Kiongozi kwa madume wenzake na Majike wengine nae ni kijakazi wa Fisi jike ambae ndio Kiongozi (Malkia) wa kundi, taarifa zote hutoka kwa Fisi Jike Kiongozi na adhabu zote hutolewa na Fisi jike.

Pamoja na yote Fisi Jike ni moja kati ya wanyama wala nyama ambae ni Parental care kwa Watoto wake, kwani ananyonyesha kwa miezi sita bila Watoto kula chochote na baadae wataendelea kunyonya kwa mwaka wakiwa wanafundishwa kula Nyama, na Fisi ndie Mnyama pekee ambae huwa anazaa Watoto wakiwa wanaona clearly uku Watoto wa Wanyama wengine huwachukua takribani week moja ndo waanze kuona, na hii ni kutokana na tabia ya Fisi kula Mifupa ambayo ina madini ya Phosphorus na Calcium.

_NATURE IS BEAUTIFUL 💖💖💖, NATURE IS INCREDIBLE 💫💫💫_

OLIVE BABOONS - NYANIWanyama hawa kila Asubuhi wanapoamka kabla ya kuanza Majukumu yao, ni lazima kwenda kumsalimia Dume...
05/05/2023

OLIVE BABOONS - NYANI

Wanyama hawa kila Asubuhi wanapoamka kabla ya kuanza Majukumu yao, ni lazima kwenda kumsalimia Dume ambaye ni Kiongozi wa Familia kwa kumkumbatia. Ingali wababe huwa hawakosekani wanaotamani nafasi yake, sababu Dume Kiongozi wa Familia anauwezo wa kuwa na jike ye yote ndani ya kundi ambae yupo tayari kuzaliana, hivyo ugomvi kwa madume mengine kuonesha uwezo wao ili waweze kumtoa karibia kila siku, wapo wezi pia ambao ni waoga hawawezi kupigana wao hupata majike kwa kuwasaidia kulea Watoto nakuonesha hali ya kuwajali zaidi Watoto wa majike hao, na hii hufanyika kwa siri sana bila Dume ambae ni Kiongozi wa Familia kujua.

WEAVERS Kwera wengi hujenga kiota na kisha kuimba katika kiota hicho ili kumvutia Jike, Jike atafika na kukagua kiota, k...
05/05/2023

WEAVERS

Kwera wengi hujenga kiota na kisha kuimba katika kiota hicho ili kumvutia Jike, Jike atafika na kukagua kiota, kikimvutia hubaki kwenye kiota hicho na asipokipenda anaweza kukivunja (kukiharibu) na kuondoka au akaondoka tu. Ikitokea amekipenda na kubaki basi Dume atajenga Kiota kingine kwaajili ya Jike mwingine.

SHARUBU - WHISKERS, TACTILE HAIR (VIBRISSAE).  Hizi ni aina ya nywele zilizonenepa nakuota kwenye uso wa Paka hasa sehem...
04/05/2023

SHARUBU - WHISKERS, TACTILE HAIR (VIBRISSAE).
Hizi ni aina ya nywele zilizonenepa nakuota kwenye uso wa Paka hasa sehemu za mdomo. K**a nywele zote zinaundwa na seli zilizokufa zilizo na keratini yenye protini.

Kazi ya sharubu kwenye uso wa Mnyama ni kuhisi na kutambua. Nywele hizi maalum husaidia kuona na kumsaidia mnyama kuzunguka na kutambua mazingira yake, na kutoa hisia za ziada, k**a vile antena kwenye wadudu.

Kila sharubu ina idadi ya seli za neva, na neva hizi hupeana maelezo ya kina kuhusu mwelekeo, kasi na muda wa harakati ya mtetemo, na hivyo kumruhusu mnyama kutambua eneo sahihi, ukubwa, umbile na maelezo mengine ya kitu au Mazingira.

NATURE IS BEAUTIFUL 💖💖💖, NATURE IS INCREDIBLE 💫💫💫

PEMBE YA FARU IMETENGENEZWA NA NYWELE.Pembe za kifaru sio pembe za kweli. Pembe za faru hazijatengenezwa kwa mfupa bali ...
04/05/2023

PEMBE YA FARU IMETENGENEZWA NA NYWELE.
Pembe za kifaru sio pembe za kweli. Pembe za faru hazijatengenezwa kwa mfupa bali ni keratini, nyenzo zilezile zinazopatikana kwenye nywele na kucha zetu. Pembe ya kifaru haijaunganishwa kwenye fuvu la kichwa chake. Kwa hakika ni wingi wa nywele zilizounganishwa ambazo zinaendelea kukua katika maisha yote ya mnyama, k**a vile nywele na kucha zetu wenyewe.

Kifaru wana sifa ya kumiliki pembe moja au mbili juu ya uso wa juu wa pua mara chache pembe tatu zinaweza kutokea.

PEMBE HII IMEUNGWAJE NA NYWELE?
Pembe za kifaru hutofautiana na pembe za kweli kwa sababu pembe hizi hazina msingi wala ala. Pembe zao huundwa na wingi wa seli za epidermal na vifungo vya papillae ya ngozi, upanuzi wa dermis. Seli kutoka kwa kila papilla huunda nyuzi za pembe sawa na nywele nene. Nyuzi hizi, ambazo zinashikiliwa pamoja na wingi wa seli za epidermal, sio nywele za kweli. Nywele za kweli hukua kutoka kwenye vinyweleo vinavyoenea hadi kwenye dermis, ilhali pembe za vifaru hukua kutoka kwenye dermal papillae zinazoenea hadi kwenye pembe.

03/05/2023

SCRUFFING

Hii ni hali au kitendo cha wanyama wengi species za Paka wakubwa na Wadogo au mbwa kubeba watoto wao nyuma ya shingo. Utaratibu huu unajulikana k**a scruffing.

Watoto wa simba huzaliwa wakiwa na ngozi nene shingoni iliyotengenezwa kwa ajili ya kubebwa. Ngozi inayojulikana k**a "scruff of the neck".

Mtoto anapobebwa atalegea kila msuli ili kumruhusu mama yake kuusafirisha hadi kwenye pango lao jipya lilo salama.

NATURE IS BEAUTIFUL 💖💖💖, NATURE IS INCREDIBLE 💫💫💫

KICHECHE.Kicheche ni mnyama anayepatikana katika bara la Afrika pekee hasa katika ukanda wa kisavana, isipokuwa kwenye m...
01/05/2023

KICHECHE.

Kicheche ni mnyama anayepatikana katika bara la Afrika pekee hasa katika ukanda wa kisavana, isipokuwa kwenye misitu mikubwa ya Congo na baadhi ya maeneo ya Afrika magharibi ambako mnyama huyu hawezi kupatikana.

Kicheche hapa nyumbani Tanzania anapatikana maeneo mengi hasa ya vijijini kwa umahiri wake wa kuk**ata kuku kwa njia ya ajabu. Kicheche ni mnyama jamii ya paka anayeishi porini ambaye kwa lugha ya kiingreza anaitwa "Zorilla" au "Polecat".

Kicheche yupo kwenye kundi la mamalia, yupo kwenye familia ijulikanayo k**a "Mustelidae" au "Weasels".
Kicheche k**a walivyo wanyama wengine wa jamii ya paka, pia yupo katika kundi la wanyama wanaokula nyama ambao kwa lugha ya kitaalamu wanaitwa "Carnivorous".

Kicheche aliyekomaa ana urefu wa sentimeta 60 tu; sawa na futi mbili, urefu ambao unajumlisha mwili na mkia, mkia pekee una urefu wa sentimeta 20.
Kicheche ni mnyama mwenye umbile dogo ila ana mbinu nyingi za kujiamini pamoja na kukabiliana na maadui zake.

Kicheche mbinu yake moja ya kujiamini na maadui zake ni kutoa harufu mbaya inayowaudhi maadui na hivyo badala ya adui kumdhuru huamua kumkimbia.
Kicheche harufu mbaya anayoitoa huzalishwa k**a kimiminika kwenye matezi maalum yaliyo kwenye sehemu yake ya kutolea haja kubwa.

Kicheche kutokana na kutoa harufu mbaya nchini Sudan inadaiwa kumuita jina la "Father of stinks" yaan baba wa harufu mbaya.

Kicheche ana tabia ya kuinua mkia wake kubinua mgongo ili aonekane mkubwa pindi anapokutana na adui yake ili amtishe.

Kicheche ni mnyama mbinafsi, wenyewe kwa wenyewe hawana tabia ya kushirikiana kwa jambo lolote isopokuwa wanapohitaji kushirikiana. Tutaendelea na somo hili ili kujua zaidi baadhi ya tabia za kicheche.
KARIBU NGORONGORO.

29/04/2023

Address

Manyara

Telephone

+255768765336

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when jeremiah_mpina posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to jeremiah_mpina:

Share