Chuma 255

Chuma 255 Blog hii ni kwa ajili ya Habari,Music na Entertaiment. [email protected] +255 712 222244

Cool and respectfull life time, out going,down to earth love making friends,i love all hate me?

29/03/2025
DAR ES SALAAM; MRADI wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) umepata sehemu ya kwanza ya ufadhili wa nje.Uf...
28/03/2025

DAR ES SALAAM; MRADI wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) umepata sehemu ya kwanza ya ufadhili wa nje.
Ufadhili kutoka kwa muungano wa taasisi za kifedha unaonesha imani katika ufanisi wa mradi huo na uwezo wake wa kuleta mageuzi katika sekta ya nishati ya Afrika Mashariki.
Washirika wa kifedha wanaounga mkono mradi huo ni pamoja na benki za kikanda k**a African Export-Import Bank (Afreximbank), The Standard Bank of South Africa Limited, Stanbic Bank Uganda Limited, KCB Bank Uganda na The Islamic Corporation for the Development of the Private Sector (ICD).
Kukamilika sehemu ya kwanza ya ufadhili ni hatua muhimu kwa EACOP na wanahisa wake.
Wanahisa hao ni Total Energies (62%), Uganda National Oil Company Limited (UNOC 15%), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC 15%) na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC 8%).
Ujenzi wa bomba hili la urefu wa kilometa 1,443 unajumuisha kilometa 296 nchini Uganda na kilometa 1,147 nchini Tanzania.

Kufikia Machi mwaka huu maendeleo ya mradi yamefika asilimia 55 na zaidi ya raia 8,000 wa Uganda na Tanzania wameajiriwa katika mradi huo.

Watoto wawili wa familia moja wa kitongoji lhula kijiji cha Bulumbaka kata Mwaubingi halmshauri ya wilaya ya Bariadi mko...
27/03/2025

Watoto wawili wa familia moja wa kitongoji lhula kijiji cha Bulumbaka kata Mwaubingi halmshauri ya wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu wamefariki kwa kudumbukia kwenye shimo la maji yanayosadikiwa kuwa na kemikali za kuchenjua dhahabu kwenye mgodi wa Gasuma no moja uliopo kwenye halmashauri hiyo.

Kaimu k**anda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Simiyu ASF Faustin Mtitu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akitaja chanzo kuwa ni kunywa maji hayo na kukosa hewa ya oksijeni.
Watoto ni wa familia moja ambao ni hao ni Yona Chai (7) na
Baraka Balida (3).

Ewe Mzalendo Taifa Stars itashuka dimbani Jumanne hii kuikabili Morocco katika mchezo wa kufuzuKombe la Dunia 2026 kwa u...
25/03/2025

Ewe Mzalendo Taifa Stars itashuka dimbani Jumanne hii kuikabili Morocco katika mchezo wa kufuzu
Kombe la Dunia 2026 kwa upande wa Afrika.
Mchezo huo utafanyika kwenye Uwanja wa Stade Municipal na utapigwa saa sita usiku kwa saa za Tanzania huku Stars ikisaka alama muhimu dhidi ya moja ya timu bora Barani Afrika.

  Hii page ina mambo mengi ndani yake ....Wasiliana nasi kupokea Tangazo Lako na Habari ya Morogoro na Picha za Matukiyo...
23/03/2025

Hii page ina mambo mengi ndani yake ....
Wasiliana nasi kupokea Tangazo Lako na Habari ya Morogoro na Picha za Matukiyo ya Mbalimbali Duniani
+255 712 222 244 Whatsapp
_________________________________
1. follow page ya
2. like picha
3. watag marafiki baada ya comment yako. .
➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖
🇳 🇯 🇴 🇴 🇲 🇴 🇷 🇴 🇹🇿 ®2025
Call us :+255 712 222244 ➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la FarajiNgomwa(33) dereva wa gari yenye namba za usajili T 120DWT aina ya HOWO amefari...
22/03/2025

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Faraji
Ngomwa(33) dereva wa gari yenye namba za usajili T 120
DWT aina ya HOWO amefariki dunia katika ajali iliyotokea eneo la Magubike wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.

Dereva huyo alikuwa akitokea jijini Dodoma kwenda
Morogoro ambapo aligonga magari mawili yenye namba za usajili T104 ARC tela namba T 376 BCG aina ya Scania likiendeshwa na Saidi Omary(65) mkazi wa Dar es salaam na gari lenye usajili T 662 EDH tela namba T 709 EDH aina ya Foton likiendeshwa na Andrea John(45) mkazi wa Lugoba.

Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro chanzo cha ajali hiyo ni dereva huyo ni kutaka kuyapita magari mengine bila ya kuchukua tahadhari.

Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika kituo cha afya
Magubike kwa ajili ya taratibu za mazishi.

DAR ES SALAAM - Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imesema bado haijakabidhi uendeshaji wake kwa kampuni ya ...
22/03/2025

DAR ES SALAAM - Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imesema bado haijakabidhi uendeshaji wake kwa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC), ikibainisha kuwa mkataba wa uendeshaji bado haujasainiwa.
Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa na Mkuu wa Mahusiano ya Umma wa TAZARA, Conrad Simuchile, mamlaka hiyo imeeleza kuwa mazungumzo kuhusu uwekezaji yanaendelea kati ya TAZARA na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, lakini hakuna makubaliano yaliyofikiwa rasmi hadi sasa.
TAZARA imewahakikishia wadau wake kuwa mara tu mchakato wa mazungumzo utakapokamilika, taarifa rasmi itatolewa kwa umma. Hii inakuja baada ya ripoti za awali kudai kuwa wachina watakabidhiwa uendeshaji wa reli hiyo kwa miaka 27.

Rais wa Burkina Faso,Kapteni Ibrahim Traoré, Alhamisi ameongoza uzinduzi wa kiwanda kipya cha saruji cha Société Industr...
21/03/2025

Rais wa Burkina Faso,
Kapteni Ibrahim Traoré, Alhamisi ameongoza uzinduzi wa kiwanda kipya cha saruji cha Société Industrielle Sino Burkina de Ciments SA (CISINOB SA) kilichopo Laongo, Ziniaré, mkoa wa Plateau-Central. Kiwanda hicho, chenye uwezo wa kuzalisha tonni 2,000 za saruji kwa siku, kinatarajiwa kuchochea maendeleo ya vianda na kutoa mamia ya ajira
kwa vijana wa Burkina Faso.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Rais Traoré alielezea mradi huo k**a ushirikiano wa heshima kati ya Burkina Faso na China, akisisitiza kuwa uwekezaji huo unalinda mamlaka ya taifa na unatoa manufaa kwa pande zote mbili.
“Kiwanda hiki ni ishara ya ushirikiano wa kweli, wenye
kuheshimu uhuru wetu wa kitaifa,” alisema Rais Traoré.
“Burkina Faso inabaki wazi kwa ushirikiano wa dhati
unaohakikisha maendeleo ya pamoja.”

Mradi huo unatarajiwa kusaidia kupunguza uagizaji wa saruji
kutoka nje, kuimarisha sekta ya ujenzi, na kuchangia katika
ukuaji wa uchumi wa taifa. Serikali imewahimiza wawekezaji
zaidi kuwekeza katika sekta muhimu ili kuimarisha maendeleo
ya Burkina Faso.

Abiria wamenusurika kifo kufuatia ajali ya basi la New Force liliokuwa linatokea Dar es Salaam kuelekea Tunduma, kugonga...
21/03/2025

Abiria wamenusurika kifo kufuatia ajali ya basi la New Force liliokuwa linatokea Dar es Salaam kuelekea Tunduma, kugongana na Malori matatu maeneo ya Mlima Nyoka jijini Mbeya, ambapo baadhi ya abiria wamepata majeraha madogo madogo.

MAMLAKA ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imetangaza kuwa Kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporati...
20/03/2025

MAMLAKA ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imetangaza kuwa Kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) itachukua usimamizi na uendeshaji wa reli hiyo kwa kipindi cha miaka 27 kwa makubaliano yenye thamani ya Dola bilioni 1.4 ambayo yatatoa fursa ya kurekebisha miundombinu ya reli na kuboresha ufanisi wake.

Mkurugenzi Mtendaji wa TAZARA, Mhandisi Bruno Ching’andu amesema sehemu ya uwekezaji utajumuisha ukarabati wa reli, pamoja na ununuzi wa vichwa vipya na mabehewa, hatua inayotarajiwa kuboresha usalama na kupanua uwezo wa usafirishaji wa abiria na mizigo.

Mkataba huu wa miaka 30 utalenga kutoa huduma bora zaidi na kudumisha operesheni za TAZARA huku Serikali za Tanzania na Zambia zikitarajia kuwa mradi huu utaongeza biashara na kuimarisha usafiri kati ya nchi hizi mbili.
Kampuni ya CCECC itasimamia uendeshaji wa reli hiyo kwa miaka 27 ijayo, huku TAZARA ikifanya kazi kwa karibu kuhakikisha utekelezaji mzuri wa mradi huu.

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imetolea ufafanuzi zoezi la utayari walilolifanya na kuonesha kuwa ndege ili...
19/03/2025

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imetolea ufafanuzi zoezi la utayari walilolifanya na kuonesha kuwa ndege ilianguka katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Taarifa yao waliyoandika katika ukurasa lao rasmi wa Instagram mara baada ya kutokea kwa taharuki hiyo imesomeka hivi:

Taharuki imetokea leo katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere kutokana na kusambaa kwa taarifa za kutokea kwa ajali ya ndege aina ya Boeing 787-9 iliyokuwa ikitokea Lanseria Afrika ya Kusini majira ya saa 1.55 asubuhi ikiwa na abiria 139 pamoja na wahudumu wa ndege.
Katika ajali hiyo kulikuwa na majeruhi na abiria waliofariki 9 ikiwa taarifa za ajali hiyo iliyotokana na shambulio la ndege hai lililopelekea hitilafu katika injini na kusababisha kuanguka kwa ndege kuwaka moto.

Maofisa kutoka vyombo mbalimbali vya dola wakiwemo Jeshi la Polisi, Jeshi la Wananchi, Uhamiaji, Zimamoto na Uokoaji, taasisi za Serikali zikiwemo Hospitali, Shirika la Msalaba Mwekundu pamoja na Wadau mbalimbali wa Kiwanja waliweza kufika mara moja eneo la tukio kwa ajili ya uokozi huku baadhi ya abiria walipoteza fahamu, majeruhi waliweza kupata msaada wa haraka kwa kupatiwa huduma ya kwanza na kupelekwa hospitali mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.

Kamishna Msaidizi na Kaimu Kamanda wa Polisi Viwanja vya Ndege Tanzania, Said Ramadhani Kitanto amesema hilo lilikuwa zoezi maalum la utayari kuona kiwanja cha JNIA kiko tayari kiasi gani katika kukabiliana na majanga na dharura.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa kiwanja hicho Bi. Bertha Bakwa amesema, zoezi hilo ni juhudi za kuimarisha usalama kwa kukabiliana na majanga na limefanyika kwa mujibu wa taratibu na miongozo ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) pamoja na miongozo ya Shirika la Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).

Pia ameendelea kusema kuwa ikumbukwe kiwanja cha JNIA ni kinara katika Viwanja Afrika kwani kiliweza kupata tuzo ya Usalama iliyotolewa na Baraza la Viwanja vya Ndege Afrika
(ACI) Septemba, 2024 hivyo ni wajibu wa Kiwanja kuonyesha kilichopatikana kinathibitishwa kwa umma kwa kuendelea kukifanyia majaribio.

Rais wa Rwanda Paul Kagame na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi, wamekutana nchini Qatar j...
19/03/2025

Rais wa Rwanda Paul Kagame na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi, wamekutana nchini Qatar jana Jumanne March 18,2025 kwa mazungumzo yao ya kwanza ya uso kwa uso tangu Waasi wa M23 waanze mashambulizi mashariki mwa Kongo mwezi January mwaka huu.

Mkutano huo umesimamiwa na Amir wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamas Al Than na ni mkutano ambao umefanyika ikiwa imepita siku moja tangu kundi la M23 lijitoe kwenye mazungumzo ya amani nchini Angola wakidai chanzo ni Viongozi wao kuwekewa vikwazo na Umoja wa Ulaya.

Kongo inaishutumu Rwanda kwa kutuma silaha na Wanajeshi wa Rwanda kuwaunga mkono Waasi wa M23 ambao mashambulizi yao yameitumbukiza mashariki mwa Kongo katika mzozo wake mbaya zaidi katika miongo kadhaa lakini Rwanda imesema kuwa vikosi vyake vinafanya kazi ya kujilinda dhidi ya Jeshi la Kongo na Wanamgambo wanaoishambulia Kigali, ikikana kuiunga mkono M23.
Wakuu hao wa Nchi wamepongeza na kuridhishishwa na hatua zilizochukuliwa kumaliza mzozo huo ikiwemo juhudi za upatanishi zinazofanywa Angola na Nairobi pamoja na mkutano wa pamoja wa EAC na SADC uliofanyika Dar es salaam Tanzania February 08,2025 ambapo Viongozi hao wote wawili wamekiri kuunga mkono makubaliano ya kusitisha vita hivyo mara moja na bila masharti k**a maazimio ya mkutano wa Dar es salaam yalivyofikiwa na wamekubaliana pia juu ya haja ya kuendelea na majadiliano yaliyoanzishwa na Doha ili kuweka misingi imara ya amani ya kudumu.

Vita vya mashariki mwa Kongo vimedumu kwa muda sasa huku madini yakitajwa k**a kichochea kikubwa cha mzozo huo ambao umeongezeka haraka tangu January 2025, na maelfu ya Watu wameuawa na wengine maelfu kulazimishwa kuyakimbia makazi yao.

17/03/2025
Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi ChanikaSP Awadh Chiko unatarajiwa kuzikwa kesho Machi 18, 2025 kati...
17/03/2025

Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Chanika
SP Awadh Chiko unatarajiwa kuzikwa kesho Machi 18, 2025 katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam baada ya kukamilika kwa taratibu za kijeshi.
SP Awadhi Chico amefariki Dunia leo Majira ya Asubuhi kufuatia Ajali ya Gari iliyotokea eneo la Pugu Sekondary baada ya Basi aina ya Eicher kugongana na gari la SP Awadh aina ya Prado wakati alipokuwa akielekea katika majukumu yake ya kila siku.

Mwili wa Marehemu SP Awadh kabla ya kuzikwa hapo kesho utaswaliwa katika msikiti wa Akachube uliopo kijitonyama na kwa sasa msiba upo Nyumbani kwakwe Kijitonyama Mtaa wa
Bukoba.

Happy birthday 🎁🎂🎊  🇭 🇦 🇵 🇵 🇾 🇧 🇮 🇷 🇹 🇭 🇩 🇦 🇾 2025Hekima ya Mungu upole na roho ya upendo ni kati ya sifa ulizokuwa nazo...
14/03/2025

Happy birthday 🎁🎂🎊

🇭 🇦 🇵 🇵 🇾 🇧 🇮 🇷 🇹 🇭 🇩 🇦 🇾 2025
Hekima ya Mungu upole na roho ya upendo ni kati ya sifa ulizokuwa nazo Leo ni siku hadhimu, siku pekee yenye history kubwa kwenye maisha yako Happy birthday to you ,Nakutakia maisha marefu na Afya | Enjoy your beautiful day ...❤🎂
➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖
🇳 🇯 🇴 🇴 🇲 🇴 🇷 🇴 🇹🇿 ®𝟐𝟎𝟐5
𝐂𝐚𝐥𝐥 𝐮𝐬 :+𝟐𝟓𝟓 𝟕𝟏𝟐 𝟐𝟐𝟐𝟐𝟒𝟒Tangaza nasi
➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖➖

Msafara wa Viongozi wa ACT Wazalendo ukiongozwa na Kiongozi wa Chama Dorothy Semu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanziba...
13/03/2025

Msafara wa Viongozi wa ACT Wazalendo ukiongozwa na Kiongozi wa Chama Dorothy Semu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Mwenyekiti wa ACT Othman Masoud Othman pamoja na msafara wa Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu, umezuiwa kuingia nchini Angola na Mamlaka za Serikali ya Angola.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa ACT, Mwanaisha Mndeme leo March 13,2025 imesema Viongozi hao wanashikiliwa katika Uwanja wa Ndege wa Luanda na hati zao za kusatiria zinashikiliwa, Serikali ya Angola, bila kueleza sababu yoyote imetoa amri y Viongozi hao kurejeshwa Tanzania.

Viongozi hao waliwasili Angola kushiriki mazungumzo ya Jukwaa la Demokrasia Afrika The Platform for African Democrats (PAD) yaliyoandaliwa na Taasisi ya The Brenthurst Foundation yaliyopangwa kufanyika kuanzia March 13-16, 2025 ambapo mbali na Viongozi hao, Viongozi wengine zaidi ya 40 kutoka nchi mbalimbali Afrika ambao pia walikuwa wanahudhuria mkutano huo wamezuiliwa na Serikali ya Angola.

Moja ya Viongozi Waandamizi waliotarajiwa kushiriki kwenye
Mkutano huo ni pamoja na Marais Wastaafu lan Khama (Botswana) na Andres Pastrana Arango (Columbia), wengine ni Waziri wa Kilimo wa Afrika ya Kusini na Kiongozi wa Chama cha DA, John Steenhuisen na Kiongozi wa Chama cha PODEMOS cha nchini Msumbiji, Venancio Mondlane.

ACT Wazalendo imelaani kwa nguvu kitendo cha udhalilishaji kilichofanyika dhidi ya Viongozi wa ACT na Vionvozi wengine kwa kuzuiliwa na kushikiliwa katika Uwanja wa Ndege wa Luanda ambapo ACT pia imemtaka Balozi wa Angola nchini Tanzania kutoa maelezo ni kwa sababu ganinViongozi hao wamezuiliwa na kunyang’anywa hati zao za kusafiriria.

“Tunaitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imuite na kumhoji Balozi wa Angola nchini juu ya kadhia hii na tunatoa wito kwa Serikali ya Angola kuziachia mara moja hati za kusafiria za Viongozi wetu walizozishikilia na kuwaruhusu kuendelea na ratiba yao nchini Angola”

#🇦🇴 #

Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limetoa sababu ya kuendelea kumshikilia bondia maarufu nchini Hassan Mwakinyo (29), anaetuh...
10/03/2025

Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limetoa sababu ya kuendelea kumshikilia bondia maarufu nchini Hassan Mwakinyo (29), anaetuhumiwa kumshambulia mkazi wa jijini Tanga M***a Ally akimtuhumu kuwa ni mwizi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo
Jumatatu Machi 10,2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amesema Mwakinyo anatuhumiwa kumshambulia na kumjeruhi M***a Ally ambae anadai ni mvuvi alipopita kwenye makazi yake.

Kamanda huyo amesema uchunguzi utakapokamilika atatoa taarifa kwa vyombo vya habari ikiwa ni sambamba na kumfikisha mahak**ani ili ajibu tuhuma zitakazomkabili.
Amesema wamemk**ata kwa tuhuma za kumjeruhi mvuvi, ambapo ni tuhuma za jinai mtu yeyote akifanya makosa k**a hayo bila kuangalia nafasi yake kwenye jamii, anatakuwa kuchukuliwa hatua za kisheria na suala la umaarufu haliwezi kubadili kile kilichotendeka.

“Jeshi la polisi Mkoa wa Tanga linamshikilia Hassan Mwakinyo (29) mkazi wa Sahare jijini Tanga kwa kumshambulia na kumjeruhi M***a Ally mkazi wa eneo hilo ambae ni mvuvi, uchunguzi wa tukio hili unaendelea na ukikamilika mtuhumiwa atapelekwa mahak**ani,” amesema Mchunguzi.

Address

Morogoro

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chuma 255 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Chuma 255:

Videos

Share