08/06/2025
⸻
Tarehe 5 Juni 2025, Taasisi ya Blue Visit Zanzibar, ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Ndg. Jasmine Kikwete, ilishiriki katika kikao maalum kilichofanyika katika Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar. Kikao hicho kilihusisha pia wajumbe kutoka Mtandao wa Twende Pamoja na Mama Sports Promotion (TPMSP).
Lengo kuu la kikao kilikuwa kujadili maandalizi ya Tamasha la “Jioni ya Almasi ya Taifa na Utulivu” pamoja na kuangazia maeneo ya ushirikiano na Wizara husika. Tamasha hili ni sehemu ya juhudi za kuunga mkono jitihada za kitaifa katika kuimarisha amani, mshikamano wa kijamii, na kukuza utalii nchini.
Katika kikao hicho, pia ilitambuliwa kwa heshima kubwa juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa mafanikio makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu
, Afya , Miundominu ya bara bara , Masoko na uchumi wa Watu
Kwa msingi huu, Tamasha la Jioni ya Almasi ya Taifa na Utulivu limeelezwa kuwa jukwaa la kipekee la kuonesha mshikamano wa kitaifa na kutoa heshima kwa viongozi waliopo kwa kazi zao kubwa za kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.