19/10/2025
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka Serikali kupitia Idara ya uhamiaji iwarejeshee hati zao za kusafiria (passport) Viongozi wa CHADEMA na iwaruhusu kuingia na kutoka Nchini k**a Raia wengine wa Tanzania.
Akiongea leo October 19,2025, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi CHADEMA, Brenda Rupia, ameeleza yafuatayo “Tunafahamu Serikali ya CCM kwa makusudi kabisa bila kueleza sababu, imetoa maelekezo maalum kwa Idara ya uhamiaji kuwazuia Viongozi wa CHADEMA kuondoka Nchini, mtakumbuka May 13,2025 katika uwanja wa Ndege wa Mwl. Nyerere Dar es salaam, Idara ya uhamiaji ilimk**ata Naibu Katibu Mkuu Bara Aman Golugwa na kuchukua passport yake na hadi leo hawajamrejeshea passport yake”
“Kwa masikitiko makubwa tunapenda kuitaarifu Serikali ya Kenya, Chama cha ODM kilichokuwa kinaongozwa na Raila Odinga na Wananchi wa Kenya kwa ujumla kuwa Chama chetu hakitoweza kuhudhuria mazishi ya Odinga kwasababu Serikali ya CCM imetuzia kuvuka mpaka wa Tanzania na Kenya”
“Pia July 12,2025 Idara ya Uhamiaji ilinizuia Mimi Brenda Rupia kuvuka mpaka wa Namanga nilipokuwa naelekea Kenya kisha Ujerumani walichukua passport yangu na hadi leo hawajanirejeshea passport yangu, pia alizuiliwa Mtaalamu wa rasilimali, miradi na uwekezaji Leonard Magele kwenda Uingereza kudhuhuria semina ya uwekezaji hadi leo hajarudishiwa passport yake”
“Tunataka Idara ya uhamiaji kupitia Serikali yake ya CCM iturejeshee passport zetu mara moja kwakuwa ni haki yetu ya kikatiba kwamba Mwananchi yeyote ana haki ya kutoka na kuingia nchini, k**a tunafuata sheria na kanuni za nchi hii kwanini tunazuiwa kutoka na kuingia nchini?” ——— Brenda Rupia.