10/07/2020
***MUNGU WA YASIYOWEZEKANA***
Kijana mmoja alikuwa anafanya kazi jeshini huku akifedheheshwa mara kwa mara kwa sababu alimwamini Mungu. Siku moja Kapteni alitaka kumfedhehesha mbele ya Askari wengine. Alimwita kijana akasema "Kijana kuja hapa, chukua funguo nenda ukapaki Jeep mbele. Kijana akajibu; "siwezi kuendesha gari! Kapteni akasema; "Naam omba msaada kwa Mungu wako! Tuonyeshe kuwa yupo!"
Kijana akachukua funguo, akaelekea lilipokuwa gari na kuanza kuomba... Alipaki Jeep mahali alipoelekezwa vizuri kikamilifu k**a kapteni alivyotaka. Kijana akatoka nje ya jeep na kuwaona wote wakilia. Wakasema kwa pamoja; "Tunataka kumtumikia Mungu wako!" Yule Askari kijana akastaajabu, akauliza "Nini kinachoendelea?" Kapteni huku akilia akafungua boneti ya Jeep na kumwonyesha kijana kwamba gari haikuwa na injini. Kijana akasema; "Umeona eh? Huyu ndiye Mungu ninayemtumikia; MUNGU WA YASIYOWEZEKANA, Mungu anayetoa uhai kwa kile kisichokuwepo." Unaweza kufikiri kuna mambo hayawezekani lakini kwa Mungu kila kitu kinawezekana. HAKUNA LISILOWEZEKANA KWA MUNGU!
Kwa wewe unayesoma hii, ninaomba Bwana atende MUUJIZA katika maisha yako leo; Katika Jina la Yesu Kristo... Andika 'Amina' au 'Amen' ukiwa na imani kuwa Mungu atatenda.
Na ikikupendeza "share" na wengine