20/10/2023
Tuliyemchangia nauli akaichungulie kesho, amerudi na majibu ya kushangaza na hadithi kibao mpya.
Anatuambia kesho watoto watawafungulia mashtaka wazazi wao, kwa-kuwa post bila ridhaa zao mtandaoni.
Kesho technology inaenda kukaa kwenye nafasi zetu.. vitanunuliwa vifaa vifanye kazi tulizosomea miaka 16 shule ya kata mpaka chuoni.
Kesho ina tahadhari kubwa, dada zetu k**a mpenzi wa bwana ako atakuwa ni mwanamke mwenzio, basi mshukuru sana mwanaume wako..
Kesho haina matumaini, wale walio dharauliwa jana tumewaona waki dharauliwa tena na kesho, kwasababu hawajakaza.
Kesho imekuja na majibu kuwa kumbe mishangazi ya leo wanaohangaika na vijana, ni wale mabinti wa jana wenye slogan ya haki sawa na ndoa zao zikawashinda.
Kesho ina kundi kubwa la wanaume waliorithi kizazi cha uchawa, shobo na kuramba miguu maboss, kinachochekewa kwenye leo ya instagram.
Kesho kwenye madhabau ya Mungu, Ajenda ya ndoa ya jinsia moja itapenyezwa kimkakati..
Kesho ya taaluma itazidi kuporomoka, shape ya kituruki na urembo wa surgery vitakupa thamani mbele ya mwenye degree yenye deni la mkopo wa Heslb mpaka leo.
"Anayejua" atapoteza ajira kirahisi mbele ya "Anayejuana na nani?"
Kesho mapenzi yatarasimishwa na mapema yataanza kulipiwa kodi k**a biashara zengine..
Kesho single mother wataongezeka na itakuwa kawaida kuzalia nyumbani..
Kesho talaka zitapokea pongezi halisi, kuliko anniversary ya miaka 10 kwenye ndoa..
Kwasababu ya leo kumiliki kizazi cha night club, viwanja, amapiano juu ya meza, nyau wa riverside na uwanja wa fisi, basi kesho watoto wengi wanaenda kupoteza baraka kwa kukosa maombi ya usiku ya mama zao..
Kesho ndo ina majibu ya ule mstari mwembamba wa ulikuwa una enjoy maisha ama ulikuwa ukiharibu future yako..
Tuingoje kesho.
OLE WETU!