04/09/2019
Mimea inayokula nyama iliopo hatararini kuangamia imeanza kupandwa tena katika maeneo kadhaa ya Uingereza katika jaribio la kupunguza kuangamia kwake.
Wataalam wa mimea wanasema kwamba mimea hiyo ilio na umbo la kuvutia imetoweka katika maeneo mengi kutokana na uhaba wa maeneo yenye ardhi zenye unyevu.
Ikiwa na mikono inayoshika na kula wadudu, mmea huo ni mmojawapo ya makumi ya mimea inayokula nyama Uingereza.
Charles Darwin alifurahishwa sana na spishi ya mmea huo , na hivyobasi kukusanya picha na vipimo katika kitabu chake kwa jina Insectivorous Plants, kilichochapishwa 1876.
Anasema kwamba alipendelea sana kuhusu mmea kwa jina Drosera, unaofahamika k**a Dawy kwa lugha ya Latin ikilinganishwa na kitovu cha spishi zote duniani.
Ni spishi ilio nadra kupatikana kulingana na Joshua Styles kutoka chuo kikuu cha Cheshire, ambaye alianzisha hisani yake ya hifadhi kwa jina North West Rare Plant Initiative kwa lengo la kuhifadhi mazingira.
Nchini Uingereza mmea huo umeorodheshwa k**a ulioangamia na hupatikana chini ya maeneo 20 hivyobasi kutopatikana kwake na hali yake kulinishawishi kutaka kuupanda tena.
Joshua Styles kushoto) akibeba mbegu ya mmea wa Sundew
Je mmea huo ni upi na unapatikana wapi?
Ulikuwa ukipatikana kwa wingi nchini England , mmea huo ulianza kuangamia katika karne iliopita.
Mabadiliko ya matumizi ya ardhi yamesababisha kukauka kwake katika maeneo yanye ardhi zilizo na unyevu.
Je mmea huo unazinduliwa vipi upya?
Joshua Styles alifanikiwa kupanda mmea huo kutokana na majani yaliokatwa yaliotoka katika mimea michache iliosalia ambayo imeweza kustahimili mazingira magumu katika eneo la Cumbria.
Alizindua mimea aina 10 katika eneo la Rsley Moss karibu na Warrington, akishirikiana na wakfu wa Chesser na ule wa wanyama pori wa Lancashire.
Mmea huo unaokula nyama unafaa kustahimili katika mazingira hayo na kuanza kuzaana.
''Kila mwaka wakati unapotoa maua unatoa makumi ya maelfu ya mbegu ndogo ndogo zinazofanana na vumbi'' , alisema.
Unapopanda 1